Natamani kuleta maagizo juu ya kutangaza Injili lakini muniruhusu nizungumzie mambo fulani! [Ndl.:Kusanyiko wanasema: Amina!].
Kwa wale wasiyo fahamu maneno ninayo yasema kuhusu William Branham, juweni kwamba ninaamini kwa ukamilifu kwamba William Marrion Branham ni nabii wa kweli aliyetumwa na Mungu Mwenyezi kwa utimilifu wa Mal.4 pia Ufu.10:7 na kwamba hata masemi yake ni sawa na ile ya manabii wa Biblia lakini siamini kwamba, hata miaka kumi tu baada ya kufa kwake, moja ya wale walio mfwata aweze kuleta hata nafsi moja tu kwa wokovu. Kuhusu maelfu za vitabu vilivyo gawanywa duniani kote kutoka Ulaya, nawaza kwamba ilikuwa tu na shabaha ya kutayarisha nafasi kwa huduma tukufu chini ya hema na kupitia hayo, ujio wa pili wa Bwana Yesu-Kristo kama vile alivyo sema mwenyewe katika muhuri wa saba. Munaona? William Branham alipo fariki, ni Tommy Osborn, mtu ambaye hakuamini hata kidogo William Branham, ndiye walimuweka mbele yao pia tarehe 11 aprili 1966, kwa kazi ya mazishi ya William Branham, ni Osborn aliye hubiri. Wale wote yaani Billy Paulo, Lee Vayle, Joseph Coleman, Perry Green, Neville na Ewald Frank walikuwa pale Tommy Osborn alipo kuwa akihubiri na kuwapa maagizo na uongozi. Hakika baada ya William Branham, kama Tommy Osborn angelipenda, angeweza kushika uongozi wa ubranhamisti hata kufikia kumupa mke wake Daisy ahubiri katika Branham maskani, kama angetaka! Kati ya makanisa ambazo William Branham alihukumu hakuna hata moja inayo weza kukubali padre mkatolika au papa aje kuhubiri kwa mazishi ya msimamizi wa kanisa lao. Haiwezekane! Osborn aliunga ndoa pamoja na Daisy tangu 1942 na hata yote anayo hubiri ni maono ya mke wake. Hakuna moja ya wale nilio wataja anaye kosa kujua mambo haya. Sasa munafahamu kwamba aina mbili kubwa kubwa za wabranhamisti ni kama ngambo mbili ya sehemu moja ya pesa! [Ndl.: Kusanyiko wanasema: Amina! ].
Na sasa ni wabranhamisti wanao sema kwamba nina huduma ya Goliatha! Je! Noa alipo kuwa akihukumu kizazi chake, akijidai kuwa peke aliye katika Kweli na hakuna aliyeweza kumpinga, je! Ilikuwa ni huduma ya Goliatha? Ikiwa hii ndiyo huduma ya Goliatha, halafu nina huduma ya Goliatha na Mungu anipe kuwa Goliatha mkuu iwezekanavyo! [Ndl.: Kusanyiko wanasema: Amina! ]. Je! Yesu-Kristo alipokuwa akihukumu watu wa wakati wake, akijidai kuwa peke katika Kweli na hakuna aliye weza kumpinga,je! Ilikuwa ni huduma ya Goliatha? [Ndl.: Kusanyiko wanasema: Amina! ]. Je! Yeye alikuwa pembe ndogo la Dan.7 linalo kufuru? Ikiwa wanazani kwamba nina huduma ya Goliatha halafu namngojea Daudi! Kore, Datan na Abiramu walipo ona kwamba Musa ana huduma ya Goliatha, walipokea zawabu yao! Wao ni wadogo na watabaki siku zote wadogo. Ile wanayo ita « mipaka ya dunia » itakuwa tu inchi yao binafsi. [Ndl.: Kusanyiko wanasema: Amina! ]. Jumapili iliyo pita, 04 mei 2008, tulibatiza kusanyiko la wabranhamisti lililo huko Dabu. Karibuni, tulibatiza kusanyiko la wabranhamisti lilo karibu nao huko Tchagba, hivyo ikatiwa mwisho kwa utawala ya Ewald Frank juu yao! Hata kusanyiko za ubranhamisti zinazo pinga ni birika zenyi kutoboka kwani watu wanatujia kutoka kule! Oh! Ujumbe tukufu, Nuru ya damani kwa mataifa! Wa sanibalati na wa tobiya hawana uwezo! [Ndl.: Kusanyiko wanasema: Amina! ]. Kama vile Adamu, Mungu alinipa mamlaka kwa kizazi hiki ili niweze kuleta majina kwa wanyama. Mungu alikaribisha nyama moja mbele yangu na niliita jina lake simba na ile ikawa jina lake. Niliwaambia waprotestanti: ninyi ni kondoo dume na ile ikawa jina yao. Nikawaambia wale wa kiinjili: ninyi ni beberu na ikawa jila yao; ila tu kama wao siyo wakatolika, waprotestanti, wa kiinjili, wabranhamisti au kinacho fanana na hao. [Ndl.: Kusanyiko wanasema: Amina!].
Kwa kumaliza na kurudi maagizoni juu ya kutangaza Injili, natamani kuwaachia wabramisti sehemu ya barua ambayo Barilier aliandikia Ewald Frank kwa 2006 ili waweze kutafakari. Ninasoma: « …Kama mahubiri ya ndugu Branham tuliyo yapokea ingepaswa kutuamsha, kama tayari tungekuwa tuliamka tokea zamani. Tambua kwamba ninasimama kwa mustari moja na wewe, kwani tangu zamani ninazidi kutafutisha kuleta tu maneno yaliyopuliziwa ya Biblia, na aibu ni kutambua kwamba mahubiri yangu kama vile yako hayakuzuiza mabikira kulala. Baba wetu wa mbinguni alijua mambo haya na ndio maana alizungumzia kelele ambayo ilibidi iamshe mabikira, hapana kwa makesha ya saba, iliyo ya mwisho, ambamo ndani mwake Roho na Bibi arusi aliye tayari anaweza kusema: Kuja! Lakini kabisa ni kwa katikati ya usiku kwani mabikira waliacha kusonga mbele… asa swali ni kujua kama tumetambua kwamba mabikira wote wamelala, sisi vilevile na kwamba mambo yale yalifika baada ya mabikira kujibu aliko la ujumbe uliyo letwa na ndugu Branham? Je! Tumetambua kwamba kama mahubiri yetu yote hayakuweza kuzuiza mabikira kulala, haya pia hayatakuwa na uwezo wa kuwaamsha, lakini Bwana aliahidi kuamsha siyo tu mabikira wenye busara, lakini pia wapumbavu, kwa kelele katikati ya usiku… kelele vilevile ni ujumbe kwani inaweza kuwa kelele inayo onyesha ujumbe wa furaha au ya huzuni, au ujumbe ya aliko kwa uamsho au kwa kujitayarisha, kama iliyo katika Mat.25:6-7. Ujumbe aliyo pewa William Branham unapaswa kutayarisha Bibi arusi. Lakini kama mabikira wanalala, namna gani wataweza kujitayarisha, namna gani wataweza kutimiza Ufu.19:7,8 na kuvaa matendo iliyo haki ya watakatifu aliyo pewa kwa kujivika? Kweli kweli Kile tunacho hitaji leo ni kuamshwa kwa kelele iliyo ahidiwa kwa saa sita manane. Yawezekana kabisa kwamba Bwana Yesu anatumia mtu mwingine mbali mbali na Ewald Frank au Alexis Barilier kwa kuamsha mabikira? Ndio, hakika!».
Hakika nitafanya safari nyingi kama ile ya Uswisi na ninawaomba wabranhamisti kuja kunisikiliza na kuniswali maulizo yote wanao taka kabla kutupilia mbali, ni ile Biblia inatuomba kufanya.
Vema, ninafikia maagizo ! Kuna inchi nyingi zilizo kwa mstari wa inchi ambazo ujumbe ni tayari ndani mwao ! wakati yule au wale wanao amini inchini moja wanaanza kufanya mikutano, inchi hiyo inaweza kutiwa kwa mustari.
Kuhusu safari yangu ya kwanza, nilichagua Uswisi kwani ndugu Arnaud ni wa kwanza kuamini inje mwa Côte d’Ivoire. Alifanya na anazidi kutenda matendo yanayo stahili yale yanayongojelewa naye. Basi si kwa sababu yeye ni mzungu; lakini namtazama kama rafiki! [Ndl.: Kusanyiko wanasema: Amina!]. Imepita siku chache, alinitumia maelezo juu ya maisha ya Darby ambayo niko nikijifunza pole pole! Na kwa kupatana, ninafurahi kuona kwamba ni kutoka Uswisi ndipo palitokea vitabu vya William Branham kwenda dunia nzima.
Sasa, ningependa niseme mambo mawili: ya kwanza, tulifanya barua ya kutangaza Injili doc. (word) inayo wezekana kutoshwa na kuiprinti toka inchi zote kwa hesabu kubwa, kuikata vipande vipande na kuigawanya popote. Dada anaweza kumupa mtu lakini mafasirio imepewa tu kwa wanaume. Natamani kuwe namba mbili ya simu au zaidi katika sehemu ya mawasiliano. Kazi hii inaweza kuanzishwa wakati kuna zaidi ya ndugu mmoja au wawili wanao elewa vizuri ujumbe na wao wanaweza kuleta maelezo iliyo wazi na majibu kwa maswali.
Ya pili, walio na mapato kidogo, kabla ya kutoa mahubiri yote kwa jumla, wanaweza kuprinti mahubiri moja kwa moja na kuigawa kwa wale wanao hitaji kufahamu ginsi wataongozwa. Kwa wabranhamisti, munajua ni mahubiri gani mutawapa na kwa wale wa kiinjili, munajua ni mahubiri gani mutawapa. Na Mungu atawaongoza na ataongoza yale mahubiri na atabariki kazi hiyo.
kurudi kwa utaratibu