MAHUBIRI N°2

TAMKA HUKUMU!

(Ilihubiriwa jumapili tarehe 18 na 25 mwezi wa nane 2002 huko Locodjro, Abidjan- Cote d’Ivoire1)



    [Ndugu Filipo anasoma Ufunuo 14:6-10: “ Kisha nikaona malaika [mwingine], akiruka katikati ya mbingu, aliye na Injili ya milele, awapashe  wanaokaa juu ya dunia, na kila taifa na kabila na lugha na jamaa, akasema kwa sauti kubwa: Ogopeni Mungu, na kumtukuza kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Mukamwabudu yeye aliyefanya mbingu na dunia na bahari na chemchemi za maji. Malaika mwingine akamfuata akisema: Ameanguka, ameanguka, Babeli mkuu, kwani amewapa mataifa yote kunywa mvinyo ya gazabu ya uasherati wake. Na mwingine, malaika wa tatu akawafuata, akisema kwa sauti kubwa: Mtu akiabudu Nyama na sanamu yake, na kupokea chapa juu ya kipaji cha uso wake, au juu ya mkono wake, yeye pia atakunywa mvinyo ya gazabu ya Mungu, iliyo wekwa pasipo kuchanganywa katika kikombe cha kasirani yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele ya Mwana Kondoo”]                                                                           

   Vema, dunia nzima inaomba daima kuhusu uamsho. Kwa kutazama umuhimu wa hitaji kama hilo, Mungu atajibu. Lakini uamsho huja tu kupitia neno la kurudishiwa. Wayahudi walimngojea Masiya lakini sawa sawa na nia yao.

    Sasa turudi kwa usomi, shairi la 6, malaika huyo anatoka wapi? Pahali neno imewekwa. Neno la Mungu latoka mbinguni    kupitia malaika lakini neno la Ibilisi latoka kuzimuni kupitia shule la uchungaji. Huyo malaika anatoka hekaluni, sawa sawa na Kanisa iliyo mbinguni, hapana katika kitabu cha Matendo ya Mitume, Vatikani, au kwa Marekani. Mungu aliifunulia Musa, Isaya, Ezekieli, na kwa manabii wote. Paulo na mitume wengine waliiona na wakaweka msingi duniani. 1Kor 3:10-11 na Efe.2:20 wanashuhudia. BASI ni wapi msingi ya makanisa zote hizo, misioni na huduma? Paulo hakuwafarakanisha wakristo wagalatia waliotaka kumtegemea ili wafanye shule ya wachungaji na teolojia? Gal.1:11-12. Leo, wabranhamisti wanafanya yote ili wabaki tu katika mafundisho ya Branham; ni mambo ya shetani! Ni zile-zile mapepo za kilutheri. Katika moja ya makutano yao, zaidi ya mbili juu ya tatu na mchungaji pia wamegeuza majina kama waislamu. Wamoja wanasema: “Tunaamini ngurumo saba…”. Wengine wanasema:”ukisema”ndugu Branham anasema” alafu”…na wengine tena:”Tunangojea mvuto wa tatu…”, “tunasema ile ambayo ujumbe inasema…”  Munaona? Wakati watu wanaacha Mungu, ni hapo wanafikia.

     Vema, tunajua ya kwamba manabii –wajumbe wote walipokea mahubiri yao toka mbinguni na tuone basi ujumbe huu wa shairi la 6 na la 7. Ni ujumbe wa kwanza unao mwambia mwafrika kwa mfano kumuabudu Yule aliye fanya dunia: nyota, jua, mwezi, hata pia wamalaika walioanguka wanao tumizia horoskope2, mambo ya maarifa, dini. Ukristu siyo dini lakini maisha. Anaomba kwa muhaiti au kwa mu benina kutoka voodoo, ufumu, asili na zingine namna zote za kuabudu na kuita roho…dunia inayowapa ninyi kuishi na ambayo munageuza kuwa pori ao msitu takatifu, sanamu na mask kwa kuiabudu…bahari na chemchemi za maji ambazo munapashwa acha kuviabudu.

    Nyuma kidogo, kwa shairi la 8, malaika wa pili alitoka siyo kwa seminari ao kwa shule ya wachungaji lakini mbiguni. Kwa kupasha teolojia? Hapana! Kwa kuenda kuwafunulia neno waalimu na wenye kufundisha katika shule za wachungaji? Hapana! Kwa kutoa maono yake kama yale mtu Fulani alisema imepita miaka makumi ine? Hapana... LAKINI WAKATI ULITIMIA KWA KUHUBIRI INJILI YA KIWANGO INGINE! [Ndl:mkutano inasema: Amina!!]. Kuhubiri hukumu ya Babeli mkuu, kanisa katolika kwa sababu alipiganisha, aliuwa watakatifu na kuchafua njia zote za wokovu. Imewekwa wazi katika Ufu.17. Ilikuwa kwa mwaka 1500 na 1600 pamoja na mapinduzi. Na ile ilifikisha mpaka uprotestanti. Baada ya hayo, wakati Lutheri, Zwingli, Farel, Kalvini, John Wesley na wengine wakafariki, makanisa zikasonga Kanisa. Mungu akapandisha sasa malaika wa tatu, mujumbe wa tatu pamoja na ujumbe wa unabii kwa wakaaji wa dunia. Mungu hasimamishi kamwe kanisa au kundi la watu kwa kuleta au kurudisha Kweli duniani lakini nabii-mjumbe. Kumkataa huyu nabii, ni kumkataa Mungu, kwa sababu nabii ni kinywa, mpitishaji-neno wa Mungu, anaye chukua ujumbe wa Mungu, mtumwa wa Mungu siyo mtu anayeleta maneno ya ujuzi au mtu anayeangusha watu chini katika makesha ya maombi pamoja na miujiza na ufunuo wa aina zote, hata kama hizo ufunuo zinakuwa kila mara kweli… Nabii, neno la kiebrania kwa nabii ni nabia na neno hilo maana yake:”mpitishaji-neno” Hapana mwenye-kubeba- miujiza au mwenye-kubeba-upako lakini “mpitishaji-neno”. Munaona? Nabii-mjumbe ni zihirisho ya neno la Mungu kwa kizazi chake. Kama huduma ya waefeso4:11 haifanyi kitu, mpango wa Mungu utatimizwa. Lakini Mungu hawezi pita pembeni, wala kubadilisha nabii-mjumbe. Hata akikataa kama Yona, hakika Mungu atamtumizia… Munaona? Na wakati nabii-mjumbe anatumwa, ni kwa sababu hakuna tena Kweli duniani na ujumbe wake inakuwa peke yake Kweli ya wakati wake. Ni yeye anashika Kweli na mwenye kutia sheria kwa neno. Munaona? Wakati Noa alikuwa akihubiri, hakuna aliye weza kuokolewa ila tu tu kwa ujumbe wa Noa. Wakati Yeremia alipokuwa akihubiri, hakuna yeyote aliye weza kuokolewa ila tu kwa ujumbe wa Yeremia. Wakati Elia alipokuwa akihubiri, hakuna yeyote aliye weza kuokolewa ila tu tu kwa ujumbe wake. Wakati Bwana Yesu alipokuwa akihubiri, hakuna yeyote aliyeweza kuokolewa ila kwa ujumbe wake. Alisema:”Hakuna anayekuja kwa baba bila kupita kwangu”. Wakati Lutheri alipokuwa akihubiri, hakuna yeyote aliyeweza kuokolewa ila tu kwa ujumbe wake. Wakati Weslei alipokuwa akihubiri, hakuna yeyote aliyeweza kuokolewa ila tu kwa ujumbe wake. Wakati William Branham alipokuwa akihubiri, hakuna yeyote aliyeweza kuokolewa ila tu kwa ujumbe wake. Na kama wewe ni mtoto wa Mungu, utawaamini na ni hivi hata leo. Na hata kabla waanze kazi, unabii za Biblia zilieleza juu yao, na kuonyesha kwamba kwa wakati Fulani, Mungu atafanya jambo Fulani. Munaona? Yesu alionyesha katika Luka 4:14-21 ya kwamba Isaya 61:1-2 ilimuhusu yeye. Yoane Mubatisti alionyesha katika Mat.3:47 ya kwamba Isaya 40:3 ilimuhusu yeye. Mtume Paulo alionyesha katika Matendo 13:47 ya kwamba Isaya 49:6 ilisemwa sababu yake… Ni ile pia tofauti kati ya manabii wa kweli na wale wa uwongo. Na kila muyuda anajua kwamba Mungu huwongoza watu wake tu kwa nabii. Na twaweza kuwa katika mapenzi ya Mungu tu kupitia nabii. Mbalimbali na wayuda ni waislamu walifahamu somo hilo. Waislamu wanaamini manabii.

    Lakini ubaya wa mtu ni kwamba hafahamu ya kuwa kuanguka katika Edeni kulimurudisha chini sana kuliko wanyama na kwamba inampasa kujitoa kwa nabii kama alivyoandika 2Mambo ya Siku 20:20…”…nao wakati walipotoka, Yosafati akasimama, akasema: munisikie, Ee Yuda, nanyi wakaaji wa Yerusalema: mwamini Bwana, Mungu wenu, ivi atawasimamisha ninyi imara; mwamini manabii wake, hivi mutasitawi…”. Munaona? Mufahamu kwamba hata mchungaji, hata huduma tano pamoja hawawezi kukamilisha Kanisa. Hata wakati wa kuchukuliwa Kutakuwa nabii-mjumbe… Munaona? Hosea 12:14 inasema: Kwa nabii Musa, Bwana akapandisha Israeli toka Misri, na kwa nabii Yoshua, akachungwa.

    Vema, malaika wa tatu anasema nini? Anahukumu siyo kanisa katoliki tu, lakini pia makanisa zingine zote, misioni, na huduma; anahukumu wale wanaojipitisha kama watumishi wa Mungu ijapo sivyo. Baadae katika hatua ya pili, anazungumzia alama ya Nyama. Ni kusema anajua ni nini alama ya Nyama na anaizungumzia. Iwe kanisa Fulani, au mtu, hata haizuru nani, hata teolojia Fulani isiwadanganye… Neno la Mungu siyo mahubiri ya kijamii, au ya mwenendo mwema, au ya elimu, au ya Injili iliyo hubiriwa imepita miaka elfu mbili lakini ufunuo ya unabii uliyo ahidiwa na Mungu kwa kizazi moja, na hiyo kwa mtu moja tu, nabii-mjumbe na huduma tano ya Waefeso 4:11 inakuwa sauti yake bila kusema tofauti naye hata kidogo.[mkutano inasema: amina].

    Naamini nimewapasha ninyi shauri la Mungu, juu ya hizo mapepo za udanganyifu ambazo watu wanaziita roho mtakatifu” ndani ya makanisa hizo za wakatolika, wametodisti, wabatisti, wa furskare, waanglikani, wanazareti, waadventisti, wamormoni, wapentekoste…na makanisa nyingi zinazo jitokeza popote. Ijapokuwa mafundisho yao ni tofauti, Shetani mungu wao iko sasa  akiwakusanya katika baraza na shirikisho ya makanisa…na miungano zingine. Na tunajua kwamba kuchukuliwa ao paradiso haiwahusu wao. Na kwa hesabu yao inafaa kuongeza sasa kundi la wabranhamisti. Na iliomba, kama majusi, niondoke Yerusalema, hiyo mchanganyikio, ili nione tena nyota. Na kila kanisa ina viungo vyengi sawa kwa wabatisti: kuna kanisa huru ya ubatisti, kanisa batisti kamilifu, kanisa batisti ya mitume, kanisa batisti ya kimisionari, kanisa batisti ya kati, kanisa batisti ya injili, kanisa batisti matendo na misioni, kanisa batisti imani na maisha, kanisa batisti kinara cha taa, kanisa batisti ya uinjilisti, kanisa ya kiinjili ya ubatisti, kanisa batisti ya pentekoste, kanisa batisti ya unabii, kanisa batisti emaus, kanisa batisti ya moto, kanisa batisti ya dunia nzima, kanisa batisti ya kristo, kanisa batisti ya wenye kuendelea, kanisa batisti iliyoundwa upya, kanisa batisti ya biblia,…zaidi ya viungo 70 na kila moja yao ina mafundisho yake ya upekee, presidenti wake, roho takatifu wake,…Biblia inasema hiyo mchanganyiko yote itaenda kwa upotevu. Kwa maana ikiwa Mungu ataokoa moja ya waliyo katika mkutano ya miungu ao mubatisti moja, basi itakuwa namna gani kwa mufarisayo, Balamu, Yuda Iskariota, na Kaina? Shetani na watoto wake wanasema: “kama wewe ni wa kanisa la wabatisti, mkutano ya miungu, uamsho ao haizuru kanisa gani na kama unaishi vizuri ile ndiyo ya lazima…” wanataka kutufahamisha kwamba katika pango la Yesu, kuna mbwa safi, mbuzi safi, nguruwe safi… lakini ni kondoo. Wanasema: “kama ulibatizwa kwa jina la baba, na la mwana na la roho mtakatifu au kwa jina la Yesu-Kristo, yote ni sawa” Lakini, Gal.1:8 inasema: alaaniwe anayesema hivi.

    Kwa Aprili 1993, kabla ya kuongoka kwangu, wakati nilipata maono mawili, ya kwanza ikielekea mwito kwa huduma na ya pili juu ya utumishi, pahali niliona imeandikwa katika mbingu ile ambayo ninahubiri leo, nilisimama katika jangwa na nikaambiwa kwamba ni jangwa ya kiroho kwani hawataweza kuniamini. Na ni kisha hayo maono mawili ndipo nilikwenda kanisani kwa mara ya kwanza. Sikujua hata kwamba ilikuwa kanisa batisti…Ninahubiri tu yale niliyoyaona siku ile upande wa saa tisa ya mchana. Hawanisadiki lakini wananipiganisha. Nge na nyoka zilizo jangwani zinanipiganisha, lakini Mungu alinipatia mamlaka juu yao na juu ya sumu yao. Wananiita pepo, mpinga Kristu, mpandaji wa mafarakano, aliyetumwa na shetani, mahubiri nivaquine… Vivyo hivyo ilikuwa kwa manabii wa Agano la Kale, kwa Yesu mwenyewe, kwa mitume… na kwa wakati wote Mungu atakapotuma watu duniani, vivyo hivyo itakavyo kuwa ili maandiko yasichanganyikiwe. Kwa Mungu Hakuna mfurugano wala kupingana kwa neno. Makuhani, wafarisayo, wasadukayo wanaungana juu ya Yesu. Luka 23:12 inasema hivi: “Siku ile Pilato na Herode wakapatana kuwa rafiki, maana mbele walikuwa na fitina kati yao.” Wandugu, nawaambia kwa jina la Bwana, mutakapoona watu waliyo na mafundisho tofauti wanaungana juu yenu, furahini! Oh! Ninyi wafarisayo wa leo, ni hakika kwamba mimi ni hatari kwa faida zenu na uakili wa kanisa zenu, lakini ogopeni Mungu!

   Jueni ya kwamba tunaishi wakati ya Loti na ya Noa ambapo makanisa walikuwa na manabii wa uwongo na watu wa upako wa aina yote walitembea duniani pamoja na miujiza ya kila aina. Wana wa upotevu waliwekwa juu ya makanisa na zehebu sawasawa na wakatolika, waprotestanti, wakiinjili pia miungano na shirikisho za makanisa… njia zote za wokovu zilikuwa mbovu. Na kwa Noa tunaona ya kwamba uzima wa milele ni kumtambua Bwana, Mungu wa kweli peke yake, na Yule inaye mpendeza kumtuma. Na waliita uarifu: hukumu. Ambacho katolika alifanya kwa wakati uliyopita, ni kile waprotestanti na wakiinjili, hiyo mfano mpya wa shetani wanakuwa wakifanya sasa. Namna gani tunaweza kuamini kwamba hizo mapepo zinazo tenda katika hizo makanisa za katolika, protestanti, pia kiinjili na wengine ni Roho Mtakatifu? Namna gani tunaweza kuwa na Biblia mikononi bila kufahamu kwamba miujiza ya hao wachawi na wafumu wenyi kuvaa koti ni tu kazi ya udanganyifu? Na hiyo uwingi wa manabii tunao waona leo wakifanya miujiza na watu wote wanashangilia. Kitambaa nyekundu kimetandikwa mbele yao. Ijapokuwa ni wale wale wananilaani; na, mahubiri yao ni ile tu wamejifunza katika kitabu cha Osborn ao cha duka ya vitabu iitwayo ya kikristo au yenye mtu Fulani wasiyomjua alitia kwenyi internet! Munaona! Na shetani alitengeneza manabii wote wa Biblia hata mpaka kuunda-unda: Abraham-Elia, Paulo-Elia, Yoani-Elia, Elia-Elisha, Ezekieli-Elia, Danieli-Elia, Samweli-Elia, Elia-Agabusi, Musa-Elia, na vivi hivi… Hakika, ni wa Elimasi na kama sivyo ni wa Yane na Yambure na miujiza zao zina shabaha la kufanya mgumu mioyo za waamini, wafarao wa makanisa na wasiwaache wayuda kutoka Misri. Na haizuru nchi gani, mutakuta majina ya manabii hawa. Haizuru pahali Fulani, dunia iko katika kiwango cha tano. Hawaoni boriti iliyo katika jicho la makanisa zao lakini wanaona kitakataka kilicho katika siasa. Watu tupu na wenye kiburi, wenye kulewa teolojia, na wenye kujiweka kwa mishituko, uchawi, na udanganyifu… wameshangiliwa kwa makanisa zote. Na tunaona makanisa zikiungana kwa aina yote ya miungano mbali na neno na hata japo wana mafundisho tofauti, wakijua kwamba mchungaji wa kusanyiko la miungu hawezi kuwa mchungaji katika kanisa la wapentekoste, la ubatisti ao waadventisti,…na kwamba moja hawezi shiriki meza ya bwana kwa mwingine. Kwa msingi gani wanaungana? Ni kwa jehanama na kwa upotevu na hayo ni kwa uanzilishi ya miungu wao na ya wale roho-takatifu wao. Oh! Ni kwa bure munaomba na kufunga chakula… Mungu atawaharibu ninyi wote. Sipendi kuwakatisha tamaa, lakini mutaenda wote kwa upotevu. Muliharibu Kweli, Mungu atawarudishia malipo yenu.

    Nilitumwa kwa kuhukumu, na niliona iliandikwa katika mbingu maneno ya hukumu juu ya kizazi kikaidi kinacho pendelea teolojia kuliko neno la Mungu, udanganyifu kuliko Kweli, Barabasi kuliko Yesu-Kristu, mauti kuliko uzima… Tunaishi wakati ya mwisho ya kuchukuliwa, baragumu za shetani zinapiga kwa ku kusanya wana wake na makanisa zake kama alivyoandika Mat.13:24-30 lakini sauti kubwa ya Mungu ya kuamuru inakusanya wateule.

    Wandugu, namna gani watu waliyo na mafundisho tofauti wanaweza kuungana? Angalieni gazeti “Fraternité matin’ ya siku ya nne tarehe 22 mwezi wa nane 2002 ukurasa 3. Wa presidenti (rais) wa makanisa mbalimbali wakijiweka pamoja mbele ya wapichaji. Kichwa cha sanamu ya joka. Wandugu, mumekwisha kuona [wapi] kundi ambayo ndani mwake kuna mbuzi, ngombe, mbwa, nguruwe, kuku… ni sanamu ya hizo miungano, baraza na shirikisho za makanisa. Na ni nani anaweza kuwa mchungaji wa kundi hilo? Hakika ni Shetani! Ngombe wanalia ouuuuhh! Mbwa wanalalamika woouuh! Woouuh! Nguruwe wananguruma grrrrhh! Grrrhh! Na mbuzi, na kuku… Munaona? Mat.13:24-30 inasema nini? “Na akawaambia: “…muyaache yakomae yote mbili pamoja mpaka wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno, nitawaambia wavunaji: okoteni kwanza magugu, na muyafunge matita kwa kuyachoma, lakini kusanyeni ngano katika gala langu”. Matita ni fungu za aina tofauti. Kanisa la wabatisti ni fungu, lakini wakati wabatisti, wamethodisti, na wengine wanajiweka pamoja, ni matita. Kila muungano au shirikisho ya makanisa ni matita. Na biblia inasema zitakuwa zengi na ni kwa kuchomwa.

    Mutakapoona wana wa shetani wakikutana na jamaa yao, wakifanya urafiki au kuungana, mutambue kwamba Mungu pia iko akikusanya wachaguliwa. Amina! Mungu alisema kwamba walipashwa fungwa pamoja kwa kuchomwa kama ilivyo andikwa katika Mat.13:24-30. Munaona pale gala ni kwa upekee lakini matita au fungu ni kwa uwingi. Munaona? Kanisa batisti huru ni fungu moja. Kanisa batisti kamili, fungu moja. Kanisa batisti ya mitume, fungu moja. Kanisa batisti ya kimisionari, fungu moja. Kanisa batisti ya kati, fungu moja. Kanisa batisti ya habari njema, fungu moja. Kanisa batisti kazi na misioni, fungu moja… Lakini, baraza la kiekumenika ya makanisa za Kenya, matita moja. Baraza la makanisa za kiinjili za taifa la Martinika, matita moja. Shirikisho la makanisa za Spanishi, matita moja. Shirikisho la makanisa za kiinjili za Ujerumani, matita moja. Muungano wa makanisa za ukarimu, matita moja. Muungano ya watumishi wa Mungu wa Ufaransa, matita moja. Munaona?

    Mungu alituma Roho Mtakatifu juu ya Matayo, Marko, Luka na Yoane na waliandika Injili nne, kila moja upande wake lakini hata mmoja hakupinga mwingine. Marko anaweza kusema kitu Fulani ambacho Yoane hakusema lakini hawatapingana hata kidogo. Shetani hawezi fanya hivyo pamoja na makanisa zake na wale roho takatifu wanao tenda katika makanisa zake. Kutoka Musa hata Paulo ilipita miaka 1600 na Mungu alipandisha zaidi ya watu 40 kwa kuandika vitabu 66 vya Biblia na munaona utaratibu? Mungu hawezi kujipinga! Hizo makanisa zote, waprezidenti wao, wareverenti wao, wachungaji na manabii... na miungu wao, roho takatifu wao na yesu wao wata kwenda wote jehanama! Niliona hayo yameandikwa mbinguni kwa aprili 1993 na niliambiwa kutamka hayo. Iliandikwa katika mbingu: tamka hukumu! Munaona?

    Ujumbe huu ni uarifu kwa wana wa Mungu ili watubu lakini wana wa Ibilisi wataiona kama hukumu na ni haki kwa maana inakuja kwa hukumu yao. Yeyote atakaye mpa moyo jirani yake ili adumu katika makanisa hizo yeye pia ataharibiwa kama mwovu, yeyote anaye hubiri teolojia ya kanisa wala hahubiri ufunuo wa unabii wa wakati wake yeye pia ataharibiwa sawasawa na Yule anaye uza vikwangara pahali pa zahabu. Aliye na masikio kwa kusikia asikie!

    Mnyanganyi mmoja alipoiba mali ya bwana wake akakwenda nchi ya mbali. Akabadilisha kitambulisho chake, na akakaa kama mtu mwema. Akaoa, akakaa katika nyumba ya bei ghali, akafanya usiano na wengi na aliwasaidia wengi. Alipopata mafasirio, bwana wake akatuma mpelelezi wa kwanza asiye mjua mnyanganyi kwa sura. Lakini alikuwa mwenye kukamilika katika upelelezi. Akakwenda, akampata lakini hakujua ya kwamba ni yule mnyanganyi. Akakaa siku nyingi kwake na akarudi na vitu vyengi alivyo pewa naye. Kisha bwana akatuma mpelelezi wa pili aliye mjua mnyanganyi kwa sura na kwa jina aliyoitwa nayo katika nchi yake ya asili. Mpelelezi akampata lakini mnyanganyi akamupa rushwa, akamupa zaidi ya mshahara ya upelelezi na akamuweka katika kazi zake za giza. Namna mpelelezi hakurudi, bwana akatuma mpelelezi wa tatu aliye mjua mnyanganyi kwa sura na kwa jina lake la kwanza. Mpelelezi alipo ona mnyanganyi na mali yake na wale aliyo wapata, akapiga kelele, akasumbua nchi nzima lakini hakuna aliye mwamini sababu ya hali na kitambulisho mpya ya mnyanganyi. Na wakaaji wa nchi ile wakashauriana kumtupa mpelelezi gerezani. Aliye na masikio kwa kusikia asikie.

1=Ivory Coast,  2= mambo ambayo watu wanafanya kwa kujua maisha yao duniani kwa wakati utakayokuja


Tuma ukurasa huu kwa rafiki

kurudi kwa utaratibu

www.matth25v6.org - Copyright © Aprili 2007
Kisheria Deposit ® All rights reserved